
Kibanda
 cha kitakachotumika wakati wa kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk John 
Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kesho kutwa kwenye
 Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Askari wa Jeshi la Wananchi akiigiza kama Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi 
nchini, Jenerali Davis Mwamunyange na mwingine akiigiza kama Rais 
anayemaliza muda wake, Jakaya Kikwete wakati wa mazoezi ya sherehe za 
kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli kwenye Uwanja wa 
Uhuru, Dar es Salaam.

  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange (wa pili kulia),
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Maangu (wa tatu kulia) na Mkuu 
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Sadick wakipiga saluti ulipokuwa unaimbwa
 wimbo wa Taifa wakati wa mazoezi ya sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu 
ya Tano, Dk John Magufuli kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.PICHA 
ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

Maofisa
 mbalimbali  wakiwa katika kibanda cha kiapo wakipanga jinsi viongozi 
watakavyokaa wakati wa sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk 
John Magufuli kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam
 

Kikundi cha sarakasi kikitumbuiza wakati wa maandalizi hayo

Wasanii kutoka Zanzibar wakicheza ngoma ya kibati wakati wa mazoezi hayo

Mtu
 aliyeigiza kama  Rais Jakaya Kikwete, akiwa amesimama alipokuwa 
akipigiwa mizinga ikiwa ni ishara ya kuagwa kwa rais huyo kabla ya 
kuapishwa Rais mpya wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli wakati wa mazoezi
 hayo.

Viongozi mbalimbali wakiwemo wa vyombo vya ulinzi na usalama wakiwa Jukwaa Kuu wakati wa maandalizi hayo.

Baadhi
 ya wananchi wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa na Bendi 
ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakati wa maandalizi hayo.

 Mtu aliyeigiza kama Rais Jakaya Kikwete, akielekea kukagua gwaride la 
heshima la kumuaga wakati wa mazoezi hayo
 
 
0 comments:
Post a Comment