Tabibu Gonzaga Marwa akiangalia baadhi ya mkopo ya Dawa jijini Dar es Salaam leo
TAASISI
 isiyo ya Kiserikali ya Tanzaone Herbal Clinic chini ya mradi wake wa 
‘Tanzaone’ hatimaye imethibitisha pasipo shaka kuwa mmea ujulikanao kama
 Lozera na bidhaa zitokanazo na mmea huo hazifai kwa matumizi ya 
binadamu na wanyama.
Akizungumza
 na waandishi wa habari, sanjari na kuonyesha majibu ya vipimo vya 
kitaalamu kutoka Wakala wa Maabara ya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa serikali 
kupitia utafiti uliofanywa chini ya mradi huo, Mratibu wa mradi.
 Tabibu
 Gonzaga Marwa, amesema  matokeo ya uchunguzi wa sampuli za mmea huo 
yameonesha una ukuvi yaani ‘fangasi’ aina ya Aspergillus ambao hutoa 
sumu ya Aflatoxin ambayo huweza kusababisha saratani ya maini.
Aidha,
 Tabibu Marwa ameiomba serikali kupitia Wizara ya Afya, na Mamlaka ya 
Chakula na Dawa TFDA, kuhakikisha wanachukua hatua za haraka kunusuru 
afya za walaji, sambamba na kushauri wadau wa tiba asili nchini kufanya 
utafiti wa kina wa dawa za mitishamba na bidhaa zake kabla ya kumfikia 
mlaji.
Hati
 ya uchunguzi ya Mradi huo, namba 241/2013, uliopewa jina la ‘Tanzaone 
Red Tea Juice’ na kudumu kwa miaka mitatu 2010/2013, kwa kushirikisha 
watuamiaji wakubwa wa Lozera zaidi ya 250 nchini kote, ilichunguzwa, 
kuidhinishwa na kuthibitishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali
 
 
 
 
 
 


 
 
0 comments:
Post a Comment