Pages

Ads 468x60px

Wednesday, December 30, 2015

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR YASAINI MIKATABA MIWILI YA UJENZI NA MAKANDARASI M/S.HUMPHREY CONTRUCTION LIMITED YA ARUSHA NA MINDSET TECHIES (T) YA DAR ES SALAAM.

 Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khadija Bakari Juma akitoa ufafanuzi kwa Wadau waliohudhuria hafla ya Utiaji Saini wa Mikataba miwili ya Ujenzi baina ya Wizara yake na Makandarasi kutoka M/S. Hamphrey Construction Limited ya Arusha na Mindset Teches (T) ya Dar es Salaam Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Elimu Zanzibar.
 Wadau mbalimbali waliohudhuria katika sherehe za kutiliana saini mikataba hiyo.
  Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khadija Bakar Juma na Mkandarasi wa Kampuni ya M/s.Humphrey Construction Limited ya Arusha wakitiliana saini Mkataba wa kupanua Taasisi ya Maendeleo ya Utalii iliopo Maruhubi.
 Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Khadija Bakar Juma na Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujenzi M/s. Humphrey Construction Limited ya Arusha wakibadilishana Mikataba baada ya kutiliana saini.

SPIKA WA BUNGE, JOB NDUGAI AMEREJEA LEO KUTOKA INDIA


SPIKA WA BUNGE, JOB NDUGAI AMEREJEA LEO KUTOKA INDIA ALIKOKUWA KWA AJILI YA MATIBABU. AWASHUKURU WATANZANIA KWA MAOMBI YAO. AELEZEA HALI YAKE KUWA NI IMARA KABISA.
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akilakiwa na Naibu Spika wa Bunge Mhe. Tulia Ackson mara baada ya kuwasili katika uwanja Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Nchini India alikokuwa kwa ajili ya matibabu.
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akilakiwa na Naibu Spika wa Bunge Mhe. Tulia Ackson mara baada ya kuwasili katika uwanja Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Nchini India alikokuwa kwa ajili ya matibabu.
  Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akisalimiana na Naibu Waziri wa Nishai na Madini Mhe. Medard Kalemani mara baada ya kuwasili katika uwanja Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Nchini India alikokuwa kwa ajili ya matibabu. Kushoto ni Naibu Spika wa Bunge Mhe. Tulia Ackson na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambula na aliyeko kulia ni Katibu wa

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo ampongeza Mbwana Samatta kwa kujiunga na klabu ya Genk ya Ubelgiji

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye(kushoto) akiongea na Mchezaji wa Timu ya TP Mazembe Mbwana Samatta(kulia) leo jijini Dar es salaam.Mbwana amemtembelea waziri Nape ofisini kwake na kuomba baraka za wizara katika kinyanganyiro cha kugombea uchezaji bora wa afrika anayechezea ligi za ndani na pia kumpa habari njema za yeye kutegemea kujiunga na timu ya Ubelgiji ya Genk.
Waziri wa Habari,Utamaduni,sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye(katikati)akiongea na waandishi wa Habari na kuwaomba watanzania kumwombea Mbwana Samatta ili ashinde katika kinyanganyiro cha kugombea uchezaji bora wa afrika anayechezea ligi za ndani kwani ni jambo la Taifa zima.Mhe Nape pia alimhakikishia kuwa Serikali ipo nyuma yake na ipo katika mkakati wa kuifanya michezo kuwa Shughuli Rasmi kwani itawafaidisha wanamichezo na Serikali kwa kupata kodi. 

Mchezaji wa TP Mazembe Mbwana Samatta(wa kwanza kushoto)akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) sababu za yeye kumtembelea Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo katika ofisi ya Wizara hiyo.Mbwana alisema kuwa amemtembelea waziri uyo kwa ajili ya kumfahamisha kuwa yumo katika kinyanganyiro cha kugombea uchezaji bora wa afrika anayechezea ligi za ndani na hivyo kuomba baraka za Wizara.Pia kumpongeza Mhe. Nape kwa kuchaguliwa kuwa waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo.Mbwana anategemea kujiunga na klabu ya Mpira ya Genk ya Ubelgiji kwa mkataba wa miaka minne.

Tume ya Mipango waaswa kufanya tafiti ili kuongeza ukusanyaji mapato.


 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akisaini kitabu cha wageni baada ya kufika katika Tume ya Mipango. Kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji Bi. Florence Mwanri.

  Baadhi ya wafanyakazi wa Tume ya Mipango wakimpokea Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango alipowatembelea kwa lengo la kuwaaga.
 Mmoja ya watumishi wa Tume ya Mipango Bw. Mohamed Ally akiongea mawili matatu na waziri mara baada ya mkutano kuisha.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Tume ya Mipango wakimpokea Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango alipowatembelea kwa lengo la kuwaaga.
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiongea na watumishi wa Tume ya Mipango alipowatembelea kwa kusudi la kuwaaga.
 Kaimu Katibu Mtendaji Bi. Florence Mwanri akimsikiliza kwa makini Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
 
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango ameiagiza Tume ya Mipango kufanya utafiti kuhusu mapato ya Serikali na namna ya kuongeza wigo wa ukusanyaji mapato.

Amesema Tume ya Mipango kama chombo cha ushauri kwa Serikali kuhusu mipango na uchumi wa nchi, ni lazima ifanye utafiti juu ya ufanisi wa ukusanyaji wa mapato na kuongeza vyanzo wa kukusanya mapato ya Serikali ili kuiwezesha Serikali kuwahudumia wananchi wake.

“Serikali isipokusanya kodi kwa ufanisi haiwezi kuwahudumia wananchi hivyo, ni lazima kodi ikusanywe ipasavyo ili kuiwezesha kujiendesha” alisema.

Dkt Mpango aliyasema hayo alipokutana na wafanyakazi wa Tume ya Mipango kwa lengo la kuwaaga baada ya kuteuliwa na Mhe. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kuwa Waziri wa Fedha na Mipango.

Waziri wa Fedha amesema mianya yote ya ukwepaji kodi ni lazima izibwe ili kuiwezesha Serikali kukusanya mapato ya kutosha suala ambalo litairahisishia utoaji wa huduma za msingi kwa wananchi.

Amesema Serikali haiwezi kutegemea kila kitu kutoka kwa wafadhili wakati nchi ina rasilimali za kutosha hivyo.Dkt. Mpango amesema Tume ya Mipango ni lazima iongoze nchi kuelekea katika uchumi wa viwanda ambavyo vitafanya pato la taifa kuongezeka na kutoa ajira kwa wananchi.

“Sisi kama wataalamu tunatakiwa kuiongoza nchi katika kufikia kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 jambo ambalo linawezekana” alisema.Waziri pia amesema ni lazima tujenge uchumi imara na madhubuti utakaowezesha kupunguza umaskini miongoni mwa wananchi.

“Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuboresha ufanisi na utendaji wa Serikali kwa ujumla hivyo ninyi kama wataalamu mna mchango mkubwa katika kutimiza hilo” alisema.

Tume ya Mipango ni chombo mahususi cha fikra rejea na ushauri kwa serikali kuhusu sera na mikakati ya maendeleo, kiuchumi na kijamii ambao unaambatana na ufuatiliaji na utathmini wa mwenendo wa uchumi nchini.

Aliwataka wafanyakazi wa Tume ya Mipango kufanyakazi kwa bidii, maarifa na weledi mkubwa ili kuimarisha utendaji Serikalini.

Monday, December 28, 2015

RAIS JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI AWAAPISHA MAWAZIRI






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli (kushoto) akimuapisha Mhe. Dkt. Philip Mpango (kulia) kuwa Waziri wa Fedha na Mipango (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge), leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli (kushoto) akimuapisha Mhe. Mhandisi Gerson Lwenge (kulia) kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji, leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli (kushoto) akimuapisha Mhe. Profesa Makame Mbarawa (kulia) (amehamishwa kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji) na kwenda Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli (kushoto) akimuapisha Mhe. Profesa Jumanne Maghembe (kulia) kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli (kushoto) akimuapisha Mhe. Dkt. Joyce Ndalichako (kulia) kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi. (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge), leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

WATU 493 WAMEFARIKI DUNIA KWA UGONJWA WA KIPINDUPINDU HAPA NCHINI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na ugonjwa wa Kipindupindu ulivyoweza kupungua ikiwa kukiwa na vifo vya watu 493 kwa Tanzania Bara.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

Na Zainabu Hamis wa Globu ya Jamii.
JUMLA ya watu 493 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa kipindupindu Tanzania bara tokea ulipoibuka jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake leo, amesema kuwa jumla ya watu 12,222 wameugua ugonjwa huo tangu ugonjwa huo wa mlipuko kuaza hapa nchini.



“Ugonjwa wa Kipindupindu umeanza tokea tarehe Desemba 15, 2015 katika mkoa wa Dar es salaam na kusambaa katika mikoa 21 ya Tanzania” Mhe. Mwalimu amesema.



Hata hivyo,Waziri huyo,amesema waathirika wa kipindupindu wameanza kupungua katika mikoa ya 
Mwanza, Arusha, Mbeya na Dar es salaam.
Pia ameitaja Iringa na Kilimanjaro kuwa ni mikoa ambayo imeweza kuthibiti ugonjwa huo hatari.

Mwalimu akitoa takwimu za ugonjwa huo, amesema hivi sasa kuna wagonjwa wapya 76, hivyo idadi ya wagonjwa wapya imefikia 493 na kifo kimoja.
“Hadi sasa mkoa wa Morogoro vijijini unaongoza kwa wagonjwa 56, ukifuatiwa na Arusha (28), Rorya (22), Bunda (21) na Kigoma vijijini 17.” Mhe. Mwalimu amesema”
Aidha Mhe.Mwalimu ametoa agizo kwa wakuu wa mikoa na wilaya kuwa ni marufuku kuuza matunda yaliyokatwa barabarani,kuuza vyakula katika mazingira yasiyo safi na salama,huku akitaka kuandaliwa kwa taarifa za kila wiki kuhusu ugonjwa huo.
Akitoa rai kwa wakuu wa wilaya na mikoa, kuwa walete taarifa sahihi za mlipuko wa ugonjwa huo kwa ajili ya kuudhibiti. Na kwa kuwasisitiza watanzania kunywa maji safi na salama na kunawa mikono kwa maji safi na salama.

Sunday, December 27, 2015

Maneno ya Edward Lowassa ma 3 akichunga Ngo’mbe alafu akaandika haya maneno 46



Edward Lowassa ambaye alikua mgombea urais kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 kupitia tikect ya CHADEMA, ameziweka hizi picha zake tatu akichunga Ng’ombe kisha akaandika haya maneno hapa chini.
>> ‘Ndugu zangu,naendelea kumshukuru Mungu kwa kila jambo. Nikiwa shambani kwangu Mzeri, Handeni nikichunga mifugo yangu naona miujiza ya Mungu ikitendeka. Mazingira ya asili ni zawadi kuu aliyotukirimu Mwenyenzi Mungu. Kila mmoja wetu kwa nafasi yake amshukuru Mungu kwa kuyathamini, kuyalinda na kuyatunza mazingira popote alipo
Lowassa 1
Lowassa 3

Friday, December 25, 2015

BONDIA THOMASI MASHALI AMKALISHA FRANSIC CHEKA MOROGORO


Bondia Thomas Mashali kushoto akioneshana umwamba na Fransic Cheka wakati wa mpambano wao uliofanyika Morogoro. Mashali alishinda kwa point katika mpambambano huo wa raundi kumi.
Bondia Thomas Mashali kushoto akikwepa konde kwa umahiri mkubwa lililorushwa na bondia Fransic Cheka wakati wa mpambano wao uliofanyika Morogoro. Mashali alishinda kwa point katika mpambambano huo wa raundi kumi.

Mabondia wa kike Lulu Kayage kushoto na Mwanne Haji wakioneshana umwamba katika mpambano wao wa ubingwa wa raundi kumi ambapo Lulu Kayage alibuka bingwa wa TPBC kwa kumpiga Mwanne kwa point. Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Lulu Kayage kushoto akimtwanga ngumi Mwanne Haji wakati wa mpambano wao wa ubingwa Lulu alishinda kwa point katika mpambano uho wa raundi kumi .

Mabondia Mwanne Haji kushoto akipambana na Lulu Kayage wakati wa mpambano wao Lulu alishinda kwa point

Bondia Vicent Mbilinyi kushoto akipambana na Deo Njiku wakati wa mpambano wao wa raundi sita Mbilinyi aslishinda kwa point mpambano huo.

Bondia Vicent Mbilinyi kushoto akipambana na Deo Njiku wakati wa mpambano wao wa raundi sita Mbilinyi aslishinda kwa point mpambano huo.

MABONDIA VICENT MBILINYI KUSHOTO SHABANI KAONEKA NA IMAN DAUDI MAPAMBANO WAKIMSHANGILIA USHINDI WA MBILINYI
 

WAZIRI NAPE NNAUYE AWATAKA WATANZANIA KUENDELEA KUMUOMBEA RAIS DK JOHN POMBE MAGUFULI, KAZI YA KUTUMBUA MAJIPU NI NGUMU NA INA VIKWAZO VINGI



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye aliyekuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Makamu wa Rais Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akizindua rasmi albam mbili za kwaya ya Wakorintho wa Pili kwenye tamasha la Krismas lililofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee leo, ambapo mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika ya Kusini Rebecca Malope amefanya onesho kubwa lililovuta hisia za mashabiki wengi waliohudhuria katika tamasha hili akishirikiana na waimbaji mbalimbali wa hapa nyu mbani na nchi jirani ya Kenya.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Nape Nnauye amewaomba watanzania kuzidi kumuombea Rais Dk . John Pombe Magufuli kwa kazi ya kutumbua majipu ambayo amekwishaianza kwani kazi hiyo ni ngumu na ina vikwazo vingi, lakini pia amewataka watanzania na waumini wa madhehebu mbalimbali kuwaombea wasaidizi wake ili waweze kuwa bega kwa bega na Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli ili kutekeleza kazi hii kwa ufanisi na kisha watanzania wafaidi matunda na rasilimali zao wenyewe.

Waimbaji kutoka Kenya walikuwa ni Faustine Munishi na Sara K na Solomon Mukubwa kutoka jiji la Nairobi huku waimbaji wa hapa nyumbani wakiwa ni Rose Muhandom Upendo Nkone, Christine Shusho, Edson Mwasabwite, Joshua Mlelwa na wengine wengi, Tamasha hilo pia lilikuwa na lengo la kumshukuru mungu kwa nchi yetu ya Tanzania kufanya uchaguzi kwa amani, Kulia ni Akex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo ndiyo imeandaa tamasha hilo.(PICHA NA JOHN BUKUKU- FULLSHANGWEBLOG-DAR ES SALAAM)
Akex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo ndiyo imeandaa tamasha hilo. akimkaribisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye ili kuzungumza na wananchi katika tamasha hilo kushoto ni Mbunge Martha Mlata na MC Mwakipesile mshereheshaji wa Tamasha hilo.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia wananchi na mashabiki waliohudhuria katika tamasha hilo katikati ni Akex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo ndiyo imeandaa tamasha hilo na kushoto ni MC Mwakipesile.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye akiimba moja ya mapambio na kuitikiwa na mashabiki wa nyimbo za injili waliohudhuria katika tamasha hilo.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye pamoja na maaskofu na viongozi mbalimbali wakishiriki katika sala maalum ya maombi iliyofanyika katika tamasha hilo,
Wamumini na mashabiki mbalimbali wa muziki wa injili wakishiriki katika maombi maalum ya kumshukuru mungu yaliyofanyika kwenye tamasha hilo.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye wakicheza pamoja na mwimbaji Upendo Nkone kutoka kulia ni Mbunge Martha Mlata na Alex Msama wakishiriki kucheza.
 
Mwimbaji Rebecca Malope akiimba katika tamasha hilo.
Waimbaji wa mwimbaji Rebecca Malope akiimba katika tamasha hilo.
Mwimbaji Rebecca Malope akiimba kwa hisia huku meza kuu pamoja na mashabiki wake wakiwa wamesimama.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye akicheza na mwimbaji Rebecca Malope wakati wa tamasha hilo. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye akicheza na mwimbaji Rebecca Malope wakati wa tamasha hilo kulia ni mbunge wa viti maalum mkoa wa mbeya Mary Majelwa na kulia ni Mbunge Martha Mlata.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye pamoja na maaskofu mbalimbali wakiwa wamesimama wakati mwimbaji Rebecca Malope akifanya vitu vyake katika tamasha hilo.
Mwimbaji Christine Shusho na Mbunge Martha Mlata wakiimba pamoja wakati wa Tamasha hilo.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye,Alex Msama na Mkewe na baadhi ya wabunge kulia ni Martha Mlata na kushoto ni Mary Majelwa wakiwa katika picha ya pamoja.
Mwimbaji Faustine Munishi kutoka nchini Kenya akiiimba katika tamasha hilo.
Wanakwaya wa Wakorintho wa pili wakiimba wimbo wao mara baada ya kuzinduliwa kwa albam zao katika tamasha hilo.
Mwimbaji kutoka nchini Kenya Solomon Mukubwa akiimba na mwimbaji mwenzake kutoka kushoto Sara K. huku mbunge Martha Mlata akishiriki kuimba nao.
Mwimbaji Joshua Mlelwa naye amefanya mambo makubwa jukwaani katika tamasha hilo.

Mwimbaji Rose Muhando pamoja na waimbaji wake wakifanya vuti vyao jukwaani.
 
Blogger Templates