Pages

Ads 468x60px

Monday, November 23, 2015

MISA TAKATIFU YA KUMBUKUMBU YA NYAMITI LUSINDE BALTIMORE, MARYLAND


 Picha ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde ikiwa kanisani siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 siku ilikofanyika misa takatifu ya kumbukumbu na kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae. Nyamiti alikua mfanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani alipatwa na mauti alipokua likizo Tanzania katika hospitali ya Kariuki alipokua amekwenda kwa matibabu baada ya kuugua ghafla alipokua huko na baadae kuaga Dunia Novemba 17, 2015. Picha na Vijimambo/Kwanza Production.

Father Honest Munishi akiongoza misa takatifu ya kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 na kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae. 

Father Lehandry Kimario akisaidiana na Father Honest Munishi katika kuongoza misa takatifu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani akiwa na mkewe Marystella Masilingi wakifuatilia misa takatifu ya kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
Balozi Mhe. Wilson Masilingi akiongea machache jinsi alivyomjua Nyamiti na kutoa shukurani zake kwa watu mbalimbali ikiwemo kamati iliyowezesha kufanikisha misa hiyo na shukurani za pekee kwa Father Honest Munishi na Father Lehandry Kimario.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates