Picha ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde ikiwa kanisani
siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 siku ilikofanyika misa takatifu ya
kumbukumbu na kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe.
Wilson Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae. Nyamiti
alikua mfanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani alipatwa na
mauti alipokua likizo Tanzania katika hospitali ya Kariuki alipokua
amekwenda kwa matibabu baada ya kuugua ghafla alipokua huko na baadae
kuaga Dunia Novemba 17, 2015. Picha na Vijimambo/Kwanza
Production.
Father Honest Munishi akiongoza misa takatifu ya kumbukumbu ya
mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 na
kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson
Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae.
Father Lehandry Kimario akisaidiana na Father Honest Munishi katika
kuongoza misa takatifu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde
iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland
nchini Marekani.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
nchini Marekani akiwa na mkewe Marystella Masilingi wakifuatilia misa
takatifu ya kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde
iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland
nchini Marekani.
Balozi Mhe. Wilson Masilingi akiongea machache jinsi alivyomjua
Nyamiti na kutoa shukurani zake kwa watu mbalimbali ikiwemo kamati
iliyowezesha kufanikisha misa hiyo na shukurani za pekee kwa Father
Honest Munishi na Father Lehandry Kimario.
0 comments:
Post a Comment