Taasisi
 ya Serious Fraud Office ya Uingereza ( SFO ) inafanya mazungumzo na 
Benki ya Standard Group ya Afrika ya Kusini Lakini iliyoorodheshwa 
katika soko la hisa ya Uingereza ( London Stock Exchange ) ili 
kumalizana kuhusu tuhuma za rushwa katika ununuzi wa hati fungani za 
Serikali ya Tanzania yenye thamani ya dola za kimarekani milioni Mia 
Sita ( $ 600m ). Mazungumzo hayo yanafanywa mbele ya Jaji katika mji wa 
London. 
Ndugu wanahabari, ni 
jambo la kawaida kwa serikali yoyote duniani kuuza hati fungani. Mnamo 
mwaka 2011/2012 Serikali kupitia Wizara ya Fedha iliuza hati fungani ( 
Bonds ) zenye thamani ya dola za kimarekani 600 milioni ($600 million), 
dhamana hizo za serikali zilinunuliwa na benki ya kigeni  (Stanbic) 
ambayo ni mali ya Standard Group ya Afrika ya Kusini, yenye makao makuu 
yake huko London, Uingereza. 
Hata
 hivyo, sehemu ya fedha hizo haikuingia kwenye akaunti za Serikali ya 
Tanzania na pia gharama za Bond hiyo zilipaishwa kupitia wakala wa kati 
kati ( middle men ) na hivyo kupelekea rushwa ya takribani $60 milioni 
kutolewa Kwa maafisa waliothibitisha biashara hiyo. 
Ndugu
 wanahabari, taasisi za kiuchuanguzi za nchini Uingereza, hasa ile ya 
kushughulikia makosa ya rushwa (Serious Fraud Office-SFO) tayari 
imeshafanya uchunguzi wake wa awali kwa kuhusisha pande zote 
zinazohusika, na wamegundua kuwepo kwa rushwa kubwa katika mchakato huo,
 jambo ambalo liliwafanya washauri uongozi wa benki hiyo hapa nchini 
kuondolewa na kurejeshwa nchini Uingereza kwa hatua zaidi. Hata hivyo 
SFO na Standard Group wanataka kulimaliza jambo hili Kwa mtindo wa 
walivyomaliza suala la radar. 
Ndugu
 wanahabari, Chama changu cha ACT-Wazalendo, kinazitaka mamlaka za 
kiuchunguzi hapa nchini, kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na 
kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote waliohusika na upotevu wa
 $600 milioni, ambazo kwa pesa ya Tanzania ni zaidi ya shilingi 1.2 
trilioni.  Hicho ni kiwango kikubwa sana cha fedha, ikilinganishwa na 
makusanyo ya Mamlaka ya Maapato Tanzania (TRA). Tunaitaka Benki Kuu ya 
Tanzania, FIU Tanzania na PCCB kuweka hadharani taarifa ya chunguzi zao 
na kueleza ni kwanini hawajachukua hatua mpaka sasa. 
Ndugu
 wanahabari, chama cha ACT-Wazalendo, kinaunga mkono jitihada za Rais 
wetu Dr John Pombe Joseph Magufuli, za kutumbua majipu, hivyo tungependa
 kuona Mheshimiwa Rais akichukua hatua kwenye jambo hili ambalo lina 
maslahi mapana ya nchi yetu, hasa ikizingatiwa na uzoefu tulionao katika
 masakata kama hayo yanayohusisha nchi za kigeni, mfano mmojawapo ni 
sakata la rada, ambalo vyombo vyetu vya uchunguzi vilisema hakukuwa na 
rushwa, na baadaye serikali ya Uingereza ilithibitisha pasina shaka 
kwamba kulikuwa na rushwa, na baadaye serikali yetu ilirudishiwa sehemu 
ya fedha zilizozidi kwenye manunuzi ya rada ( chenji ya rada ). 
Chama
 cha ACT Wazalendo kinasubiri taarifa ya makubaliano ( settlement ) Kati
 ya SFO na Benki ya Standard Group ( Benki mama ya Stanbic ) ili 
kushauri zaidi hatua za kuchukua. Ikumbukwe kuwa Benki ya Stanbic ndio 
ilihusika na kashfa ya Tegeta Escrow na mpaka sasa haijachukuliwa hatua 
zozote kama ilivyoagizwa na Bunge. Benki hiyo imewaficha waliochota 
fedha za escrow mpaka Leo. 
( imesainiwa ) 
Masasi, 30 Novemba 2015
Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto, Mb
ACT-WAZALENDO
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment