Washiriki
 wa warsha hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na mwakilishi wa mgeni 
rasmi ambaye ni mshauri wa mradi huo Bw. Ahmed Athumani.
Mwakilishi
 wa Mkurugenzi wa Soko la Ajira ,Mipango na Maendeleo wa VETA, Ahmed 
Athuman akizungumza katika warsha ya wadau wadau wa viwanda,umeme na 
magari kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa 
ushirikiano kati VETA na wadau hao iliyofanyika katika ukumbi wa 
Giraffee Hoteli jijini Dar es Salaam.
Sehemu
 ya wadau wakifatilia maada mbalimbali katika kujadili utekelezaji wa 
mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano kati VETA na wadau hao 
iliyofanyika katika ukumbi wa Giraffee Hoteli jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii
MAMLAKA
 ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)imekutana na wadau wa 
viwanda,umeme na magari kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo 
yanayotolewa kwa ushirikiano kati yake na viwanda.
Akizungumza
 na wadau wa mamlaka hiyo wakati akifungua warsha hiyo Mwakilishi 
wa Mkurugenzi wa Soko la Ajira ,Mipango na Maendeleo wa VETA, Ahmed 
Athuman alisema moja ya sababu zinazokwamisha ajira kwa vijana nchini ni
 ukosefu wa mafunzo ya vitendo kwa vijana wanaohitimu katika taasisi 
mbalilmbali unaosababishwa na kutokukwepo kwa ushirikiano thabiti kati 
ya Taasisi za Mafunzo na Viwanda.
Amesema
 kuwa VETA inatoa mafunzo yatakayomuwezesha muhitimu kuajiriwa 
au kujiajiri kutokana na mafunzo ya vitendo yanayotolewa kutokana na 
mahitaji yaliyopo nchini 
Ahmed
 amesema kuwa ushirikiano wa wadau utaleta matokeo chanya kwa vijana 
kuweza kufanya kazi kutokana mafunzo walioyapata katika taasisi za 
mafunzo ya ufundi Stadi.
 
 
 
 
 
 



 
 
0 comments:
Post a Comment