Kaimu 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Maji, 
Athumani Sharif akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo 
pichani) kuhusu mikakati ya Serikali kutatua tatizo la upatikanaji wa 
maji jijini Dar es Salaam mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto 
ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa. 
(Picha na Fatma Salum.)
Na. Georgina Misama - Maelezo
SERIKALI
  inatarajia kuzalisha maji lita milioni 270 kwa siku baada ya 
kukamilika kwa mradi wa upanuzi wa Chanzo cha Maji cha Ruvu Chini na 
upanuzi wa mtambo wa kusafishia maji.
Mradi 
huo  unaotekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimarekani
 la Millenium Challenge Co-operation umegharimu kiasi cha shilingi 
bilioni 66.24 na unatarajiwa kukamilika wakati wowote baada ya 
kukamilika kwa kazi ya kulaza bomba linalosafirisha maji toka Ruvu chini
 kuja Jijini Dar es Salaam.
Akiongea
 na waandishi wa habari, leo Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha 
Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Maji, Bw. Shariff Athumani 
amesema kwamba mradi wa upanuzi wa mtambo wa ujenzi wa bomba la Ruvu 
Chini utapunguza kero ya maji kwa wakazi wote wanaotumia maji kutoka 
Ruvu Chini.
Akiyataja
 maeneo yatakayofaidika na kukamilika kwa mradi huo ni pamoja na 
Bagamoyo na vitongoji vyake, Bunju, Mabwepande, Boko, Tegeta Kunduchi na
 Mbezi Beach. Maeneo mengine ni pamoja na Mbezi Juu, Salasala, Kawe, 
Makongo, Chuo Kikuu, Mikocheni, Msasani, Masaki, Mwananyamala, 
Kinondoni, Magomeni, Sinza, Manzese, Ubungo, Mabibo, Kigogo, Buguruni, 
Ilala, Kurasini, Bandarini na maeneo yote ya katikati ya jiji la Dar es 
Salaam.
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment