Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla akiwaamrisha askari wa getini wizarani hapo kuweka 
kufuli na kutoruhusu mtumishi yoyote wa ofisi hiyo kuingia ndani ya 
ofisi za wizara ilipotimu saa 1:32 asubuhi mapema leo.(Picha zote na 
Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla akisimamia zoezi la ufungwaji wa geti hilo, Kulia ni
 askari wa SUMA JKT akiweka kufuli katika lango kuu la kuingia katika 
ofisi za Wizara ya Afya.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla akiwauliza askari wa getini kuhusu daftari la 
mahudhurio ya watumishi wa wizara baada ya kufungwa geti hilo, na kupewa
 maelezo kuwa watumishi huonyesha vitambulisho pekee na husaini katika 
vitengo vyao.
Mmoja
 wa wafanyakazi wa Wizara ya Afya akiwasili ofisini huku muda wa kuingia
 kazini ukiwa umepitiliza. Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
 Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akizungumza na
 mmoja watumishi wa wizara hiyo na kuagiza kuletewa vitabu vya 
mahudhurio kwa vitengo vyote vilivyopo wizarani hapo.
Mkurugenzi
 wa Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Afya, Michael John 
akitoa maelezo kuhusu mahudhurio ya watumishi kwa Naibu Waziri wa Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla.
Magari
 ya watumishi wa Wizara ya Afya yakiendelea kuwasili ofisini bila ya 
kutambua kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri, Dkt. Kigwangalla ametoa agizo la 
kuizuia watumishi wachelewaji.
Askari
 wa getini wakimpa maelezo mmoja wa watumishi wa wizara hiyo  kuwa Mh. 
Naibu Waziri ameagiza watumishi wote waliochelewa kuzuiliwa kuingia 
ndani. 
Mmoja
 wa wasaidi wa idara ya rasilimali watu akimkabidhi vitabu vya 
mahudhurio Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na 
Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla akipitia mahudhurio ya watumishi wa wizara kwa siku 
zilizopita.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla akipitisha mstari wa kufunga mahudhurio kwa 
watumishi ambao wameripiti kabla ya saa 1:30 asubuhi ya leo.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla akiendelea na zoezi hilo la kupitisha mstari kwa 
kila idara za wizara hiyo.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla akizungumza na waandishi wa habari kuhusu juu 
ukaguzi huo katika ofisi za wizara yake ya afya ili kuboresha utendaji 
wa wizara hiyo na vituo vyote vya sekta ya afya nchini kote.
Na
 Rabi Hume, Modewjiblog
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kingwangalla amefanya ukaguzi wa kushtukiza katika ofisi za 
wizara hiyo kwa kusimama getini kuzuia wafanya kazi wote wa wizara ambao
 walikuwa wamefika ofisini baada ya saa 1:30 asubuhi  muda ambao ndiyo 
mwisho wa wafanyakazi kuingia ofisini. 
Awali
 Dkt. Kingwangalla alifika ofisini saa 1:05 asubuhi huku akiingia 
ofisini kwa kutembea mwenyewe bila kutumia usafiri wa gari na kwenda 
moja kwa moja ofisini kwake ambapo alitoka ilipofika saa 1:32 na kwenda 
kusimama getini na kisha kuwaamrisha askari wa geti la kuingia katika 
wizara hiyo kulifunga geti hilo na wasiruhusu mtu yeyote kuingia ndani.
“Fungeni geti na kila atakayefika msimruhusu kuingia ndani ninataka 
kuona wote ambao wanakuja wamechelewa,” alisikika Dkt. Kingwangalla 
akiwambia askari wa getini. 
 Baada
 ya kutoa amri hiyo alimtaka Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa
 wizara hiyo, Michael John kumpa vitabu vya kusaini kwa vitengo vyote 
ili aweke mstari wa kuonyesha kuwa muda wa kuingia ofisini umekwisha na 
akafanya hivyo kwa kuweka mstari kwenye vitabu vya mahudhurio kuwa muda 
wa kusaini kuingia umeisha. 
Baada
 ya kukamilisha zoezi hilo Naibu Waziri alizungumza na wanahabari kuwa 
ameamua kufanya zoezi hilo katika ofisi za wizara kwa kutaka kuona ni 
jinsi gani watumishi wa ofisi hiyo wamekuwa na mwitikio wa kufanya kazi 
kwa kasi anayoitaka rais, Dkt. John Pombe Magufuli.
Alisema watumishi hao wameajiriwa na serikali ili kufanya kazi lakini 
wamekuwa wakichelewa kuingia ofisini na yeye kama Naibu Waziri ana 
wajibu wa kuwasimamia watumishi hao ili wafanye kazi ambayo serikali 
imewaagiza kufanya. 
“Nina
 wiki moja tangu nimeingia hapa ofisini kuna mambo ambayo nimeyaona 
hayapo vizuri na sasa naanza na hili ili tujue kuwa  ni kina nani huwa 
wanachelewa na zoezi hili litakuwa ni endelevu, kama mimi sitasimamia 
watumishi wa serikali basi sitakuwa na kazi wizarani tunataka watumishi 
ambao wanakuwa wanafanya kazi kwa kujitoa kwa ajili ya maslahi ya 
taifa,” alisema Dkt. Kingwangalla. 
 Aidha
 Naibu Waziri huyo alimtaka Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu 
kuhakikisha watumishi wote waliochelewa kufika ofisini wanaandika barua 
ya kutoa maelezo kwanini wanachelewa kufika ofisini na baada ya hapo 
Mkurugenzi na yeye atoe maelezo kwanini muda wa kutoka watumishi 
wanakuwa hawasaini kuwa wametoka. 
 Pia
 alishauri uongozi wa wizara ufanye mabadiliko ya mfumo wa watumishi 
kuingia ofisini kwa kutumia mifumo ya kisasa ya kadi au kidole 
“Biometric” ili kuwa na taarifa katika mifumo ya mawasiliano kujua 
wanaochelewa ofisini na wanaowahi kutoka na baada ya hapo uongozi 
utajadili adhabu za kuwapa watumishi wote ambao wamekuwa wakichelewa 
kufika na kuwahi kutoka ofisini.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment