Mkurugenzi wa barabara Wizara ya 
Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Ven Ndiyakumana kushoto 
akisaini mkataba wa awali kuhusu mkopo wa fedha wa riba nafuu 
utakaosaidia ujenzi wa Barabara ya Arusha hadi Holili kulia ni Naibu 
Mkurugenzi wa Idara ya ushirikiano Afrika kutoka Japan (JICA) Bw. 
Hideyuki Manioka wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo Jijini Dar es 
salaam.
Mkurugenzi wa barabara Wizara ya 
Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Ven Ndiyakumana kushoto 
akikabidhiana mkataba wa awali kuhusu mkopo wa fedha wa riba nafuu 
utakaosaidia ujenzi wa Barabara ya Arusha hadi Holili na Naibu 
Mkurugenzi wa Idara ya ushirikiano Afrika kutoka Japan (JICA) Bw. 
Hideyuki Manioka wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo Jijini Dar es 
salaam.PICHA ZOTE NA ALLY DAUD-MAELEZO
…………………………………………..
Na Raymond Mushumbusi Maelezo
Serikali ya Tanzania kupitia 
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano leo imesaini mkataba wa 
makubaliano ya awali ya ujenzi wa barabara kutoka Arusha mpaka Holili.
Makubaliano hayo yamesainiwa na 
Mkurugenzi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano 
Mhandisi Ven Ndyamukama kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Naibu 
Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano (JICA) Bw Hideyuki Manioka  kwa niaba ya
 Serikali ya Japan.
Mhandisi Ven Ndyamukama amesema 
kuwa Tanzania imesaini mkataba huu wa awali ambao baada ya majadiliano 
ya awali kati ya Tanzania na Japan, serikali ya Japan itatoa mkopo wa 
riba nafuu kwa serikali ya Tanzania ili kuwezesha kuanza kwa utekelezaji
 wa mradi huu mapema marchi mwakani.
“Wamekuja kufanya utafiti na 
kufatilia taarifa tulizo nazo kuhusu mradi huu na kupeleka taarifa 
serikali ya Japan na tunategemea June mwakani kusaini hati ya kupata 
mkopo ambao utawezesha ujenzi wa barabara hii ” Alisema Mhandisi 
Ndyamukama.Pia ameongeza kuwa baada ya 
mkopo huo kutolewa wao kwa upande wao wamejipanga katika kufanya mradi 
huo ukamilike kwa wakati ikiwemo upatikanaji wa wakandarasi kwa ajili ya
 mradi huo. 
Aidha Naibu Mkurugenzi wa Idara 
ya Ushirikiano (JICA) Bw Hideyuki Manioka  amesema kuwa wataendelea 
kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kusaidia miradi mbalimbali 
ya maendeleo.
Mradi huu wa barabara toka 
Arusha mpaka Holili  yenye urefu wa kilometa105 umefadhiliwa na Serikali
 ya Japan kupitia Wakala wa mambo ya Ujenzi(JICA) na unatarajiwa kuanza 
mapema mwakani,hii ikiwa ni juhudi za Serikali katika kuboresha 
miundombinu hasa ya barabara kwa kuzifanya barabara nyingi nchini kuwa 
katika kiwango cha lami.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment