Kijiji cha Magozi chenye wakulima 
zaidi ya 1000 wanaolima mpunga kwa kutumia kilimo cha  umwagiliaji ambao
 unasababisha bwawa la mtera kukosa maji kutoka mto Ruaha kwa sababu za 
kilimo cha umwagiliaji. Pamoja na wakulima Hawa pia wapo wakulima  wa 
Mbalali mkoa wa Mbeya ambao wote kutokana na shughuli hizo za kilimo 
husababisha ufuaji umeme kukwama katika bwawa la  Mtera na Kidatu 
 mkoani Morogoro.
Waziri wa Nishati na Madini 
Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo kushoto anayezungumza na Richard 
Kasesela Mkuu wa wilaya ya Iringa  alitembelea  bonde hilo na kukagua 
shughuli za kilimo zinazoendelea katika bonde hilo na kusababisha 
upotevu wa maji katika mto Ruaha ambao unapeleka maji katika mabwawa ya 
kufua umeme Mtera, Mkuu wa wilaya ya Iringa ameitisha mkutano wa wadau 
wote  siku ya jumatatu tarehe  21 mwezi huu . ili kufanya majadiliano na
 kupanga mkakati wa Kuokoa bwawa la mtera.
Waziri wa Nishati na Madini 
Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo akikagua eneo hilo na Mkuu wa Wilaya 
ya Iringa Mh. Richard Kasesela leo.
Waziri wa Nishati na Madini 
Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo akizungumza na baadhi ya wakulima hao
 wakati alipokagua bonde hilo kulia anayemsikiliza ni Mkuu wa wilaya ya 
Iringa Mh. Richard Kasesela.
Waziri wa Nishati na Madini 
Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo akizungumza na mkuu wa wilaya ya 
Iringa Mh. Richard Kasesela wakati alipotembelea bonde la Usangu lenye 
shughuli za kilimo cha Umwagiliaji.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh. 
Richard Kasesela akimwelezea jambo waziri wa Nishati na Madini wakati 
alipokagua bonde la Usangu katika kijiji cha Magozi chenye wakulima wa 
mpunga zaidi ya 1000.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment