Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Ummy Mwalimu akipokea taarifa ya 
makabidhiano ya ofisi na aliyekuwa Waziri wa iliyokuwa Wizara ya Afya na
 Usatawi wa Jamaii ya Serikali ya Awamu ya Nne Dkt. Seif Rashid wakati 
wa kukabidhiwa rasmi ofisi leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Ummy Mwalimu akimsikiliza aliyekuwa 
Waziri wa iliyokuwa Wizara ya Afya na Usatawi wa Jamaii ya Serikali ya 
Awamu ya Nne Dkt. Seif Rashid wakati wa kukabidhiwa rasmi ofisi leo 
jijini Dar es salaam.
Aliyekuwa Waziri wa iliyokuwa 
Wizara ya Afya na Usatawi wa Jamaii ya Serikali ya Awamu ya Nne Dkt. 
Seif Rashid (kushoto) akisalimiana na Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya
 Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangala (kulia) leo 
jijini Dar es salaam.
……………………………………… 
NA Eleuteri Mangi-MAELEZO
Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Ummy Mwalimu amekabidhiwa rasmi ofisi na 
aliyekuwa Waziri wa iliyokuwa Wizara ya Afya na Usatawi wa Jamaii ya 
Serikali ya Awamu ya Nne Dkt. Seif Rashid leo jijini Dar es salaam.Akipokea ofisi hiyo, Waziri Ummy 
alimshukuru Dkt. Seif kwa jitihada kubwa waliyofanya ya kupambana na 
magonjwa kwa wananchi na kufanikisha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi 
duniani ambayo imetatua tatizo la ugonjwa wa polio na kuwa “polio free”..
Aidha, Waziri Ummy amemhakikishia 
Dkt Seif kuendelea kushirikiana naye pale msaada wake utakapohitajika 
kwa kuwa anauzoefu katika masuala ya afya ili kuwahudumia Watanzania na 
kupambana na adui wa taifa ambaye ni magonjwa.Akikabidhi ofisi, Dkt Seif 
aliwapongeza Waziri Ummy Mwalimu na Naibu wake Dkt. Hamisi Kigwangalla 
kwa kupewa nyadhifa hizo na kuahidi kuwapa ushirikiano wake 
paleutakapohitajika.
Dhana ya “Hapa Kazi Tu” imechukua 
mkondo wake ambapo hadi sasa Mwaziri na Manaibu waziri wanatekeleza 
dhana hiyo kwa vitendo na siyo kukaa ofisini, kwa kwa juhudi hizo 
viongozi kwa kushirikiana na wananchi, Tanzania itafanikiwa kufikia 
uchumi wa kati ifikapo 2025 ikiwa na watu wenye afya bora inayowaruhusu 
kufanyakazi kwa juhudi na maarifa ili kuwa maendeleo yenye tija kwa 
Wtanzania.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment