Ni majira 
ya saa 10 na dakika 10 Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo 
ndipo alipofika katika mitambo ya kuzalisha umeme wa gesi ya Tegeta 
jijini Dar es Salaam kinachomilikiwa na Tanesco bila ya kutoa taarifa na
 kukuta wafanyakazi pamoja na wahandisi wa kituo hicho cha umeme 
wakiendelea na kazi katika mitambo hiyo. 
Na kukagua
 mitambo hiyo leo  na kubaini kuwa umeme uniti moja inatengenezwa kwa 
gharama ya shilingi 90 na kuuzwa kwa wananchi kwa shilingi 180 ikiwa ni 
kiwango kikubwa kwa mwananchi wa kawaida.
Pia Mhongo amesisitiza kuwa umeme unatakiwa kushuka bei ili kila mwananchi anufaike na umeme hapa nchini.
Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo akipokea vifaa vya 
kuzuia kusikia sauti kuingia masikioni mara baada ya kufanya ziara ya 
kushtukiza katika Mitambo ya Gesi ya Tegeta jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo akizungumza na Meneja
 wa Mitambo ya gesi ya Tegeta jijini Dar es Salaam, Mohamed Kisiwa mara 
baada waziri wa Nishati na Madini kutembelea mitambo ya umeme wa gesi wa
 Tegeta jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo akipewa maelekezo na 
Meneja wa Mitambo ya gesi ya Tegeta, Mohamed Kisiwa mara baada ya waziri
 huyo kutembelea mtambo huo bila kutoa taarifa na kuhoji baadhi ya 
matengenezo katika mtambo huo.
Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo akitembezwa na Meneja
 wa Mitambo ya gesi ya Tegeta Mohamed Kisiwa mara baada ya kutembelea 
mitambo ya Tegeta jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Mitambo ya Gesi iliyotembelewa na Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo akipewa maelekezo na 
Meneja wa Mitambo ya gesi ya Tegeta, Mohamed Kisiwa jijini Dar es Salaam
 leo.
 
 
 
 
 
 











 
 
0 comments:
Post a Comment