Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akiwasili katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipofanya 
ziara ya kushtukiza hospitalini hapo, Januari 4, 2016.(Picha zote na 
Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo
 ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi Kingwangalla 
amefanya ziara, Januari 4, 2016 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili 
na kutembelea idara mbalimbali za hospitali hiyo kuona jinsi  ya 
ufanyaji kazi.
Baadhi ya idara ambazo,  Dk. Kingwangalla
 alitembelea ni pamoja na Kitengo cha dharura, Chumba cha wagonjwa 
Mahututi (ICU), wodi ya Mwaisela, duka la dawa la MSD na kukagua 
ufanyaji wa kazi wa mashine ya CT-Scan na MRI.
Akizungumzia ziara hiyo mara baada ya 
kutembelea Hospitalini hapo, Dk. Kigwangalla  ameeleza kuwa ili kuweza 
kuona hali ya utendaji wa kazi iliyopo katika hospitali hiyo ya taifa 
tangu ambapo Rais, Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya 
kushtukiza na kutokuridhishwa na utendaji kazi wa hospitali hiyo hali 
iliyopelekea kuivunja bodi iliyokuwa ikisimamia hospitali.
Dk. Kingwangalla alisema amefurahishwa na
 utoaji wa huduma katika upimaji kwa kutumia mashine ya CT-Scan na MRI 
ambazo awali wakati wanaingia madarakani hazikuwa katika hali nzuri ya 
ufanyaji wa kazi na kuwataka watumishi wa hospitali hiyo kufanya kazi 
kwa bidii na kuifanya hospitali hiyo kuonekana yenye hadhi ya kuwa 
hospitali ya taifa.
Alisema limekuwa jambo ambalo 
linasikitisha kuona huduma zinazopatikana katika hospitali ya taifa 
zinashindwa na huduma zinazotolewa katika hospitali za watu binafsi na 
akilinganisha huduma za kulipia vitanda zinazotolewa Muhimbili kuwa 
hazina viwango vya juu ambavyo vinaweza kuwashawishi wananchi wenye 
uwezo kuacha kwenda hospitali binafsi na kwenda hospitalini hapo.
“Ni jambo la kushangaza hospitali za watu
 binafsi zinakuwa na watu wengi kuliko hapa na wakati sisi tuna 
madaktari bingwa zaidi ya 500 hapa Muhimbili lakini hizo hospitali zao 
hazina hata daktari mmoja bingwa lakini na huduma zinazopatikana katika 
madaraja ya juu zinatakiwa kuboreshwa,
“Kama tunaweza kuwa na huduma nzuri 
katika first class (daraja la kwanza) tunaweza kuwavuta wananchi wengi 
waje hapa na waache kwenda hospitali binafsi, wanatakiwa kutengwa 
madaraja ya juu ambayo huduma zake zinakuwa zimeboreshwa sio mtu anakuwa
 daraja la kwanza alafu bado anachangia choo na wengine au anaelala nae 
hapewi kitanda,” alisema Mhe. Kingwangalla.
Aidha Mhe. Dkt.Kingwangalla aliwatupia 
lawama Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa jinsi wanavyopanga 
madaraja ya hospitali na kuilinganisha Muhimbili na hospitali zingine za
 watu binafsi kuwa jambo hilo siyo sahihi kwa kuiweka hospitali ya taifa
 sawa na hospitali za watu binafsi.
“NHIF wanaweka sehemu moja hospitali ya 
taifa na hospitali binafsi hili haliwezekani walinganishe huduma 
zilizopo hospitali ya taifa na zile zingine, nina mpango wa kuwatembelea
 hivi karibuni nitazungumza nao,” alisema Kingwangalla.
Aidha Mhe. Naibu Waziri aliupongeza 
uongozi wa hospitali hiyo kwa kuongeza vitanda katika wodi ya wagonjwa 
mahututi (ICU) ambayo awali ilikuwa na vitanda sita hali ambayo ilikuwa 
ikiwashangaza wananchi wengi kutokana na kuwepo kwa vitanda zaidi ya 
1350 katika hospitali hiyo na hivyo kuongezeka kwa vitanda katika wodi 
hiyo kutasaidia upatikanaji wa wa huduma bora kwa wagonjwa wanaofika 
hospitalini hapo kupata huduma.
Awali akitoa taarifa mbele ya Mhe. Dkt. 
Kingwangalla, Mkuu wa Idara ya Mionzi katika hospitali hiyo, Dkt. Flora 
Rwakatare alisema tangu kuanza kwa kutumika kwa mashine ya MRI mwishoni 
kwa mwezi Novemba mwaka jana jumla ya wagonjwa 560 wamefanyiwa vipimo 
katika mashine hiyo na ndani ya siku tatu amabazo wamefunga mashine mpya
 ya CT-Scan wameshawapima wagonjwa 26.
Alisema kufungwa kwa mashine ya CT-Scan 
kunaonekana kuwepo kwa matumaini mapya kwa watanzania kutokana na kasi 
ya ufanyaji kazi kwa mashine hiyo ambayo imetengenezwa na kampuni ya 
Siemens ambayo inauwezo wa kupima kifua na tumbo kwa sekunde 6.
“Mashine ya CT-Scan ambayo imefungwa ina 
ubora mkubwa na ni ya pili kwa ukubwa Afrika Mashariki na kwasasa 
tunategemea kufanya kazi kwa ubora zaidi kutokana na ukubwa iliyonayo na
 inaweza kufanya kazi kwa kasi tofauti na ile iliyokuwa ikitumika 
awali,” alisema Dkt. Flora.
Nae Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya 
Taifa ya Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru alisema awali hawakuwa 
wakifanya visingizo ili wasifanye kazi lakini ni hali halisi iliyokuwepo
 kuwa mashine iliyokuwepo awali ilikuwa na matatizo lakini kufanikisha 
kufungwa kwa mashine mpya ambayo imeigharimu serikali Dola za Kimarekani
 Milioni 1.7 ambapo ni zaidi ya Milioni 400 za kitanzania kutawapa wao 
motisha ya kufanya kazi kwa kutumia kifaa cha kisasa na chenye kufanya 
kazi kwa haraka.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akitoka katika ofisi ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa 
Hospitali hiyo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya 
Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru (kushoto). Katikati ni Mkuu wa Idara ya 
Magonjwa ya Dharura na Ajali ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya
 dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Juma Mfinanga.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akiongozana na Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya 
Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru (kushoto) pamoja na Mkuu wa Idara ya 
Magonjwa ya Dharura na Ajali ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya
 dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Juma Mfinanga 
(kulia) kuelekea kwenye chumba cha vipimo vya CT Scan pamoja na MRI 
alipofanya ziara ya kushtukiza hospitalini hapo, Januari 4, 2016.
Baadhi ya watumishi katika kitengo cha 
vipimo cha MRI wakiandaa kitanda kwa ajili ya kumpokea mgonjwa wa kipimo
 cha MRI (hayupo pichani) kama walivyokutwa na mpiga picha wa wetu.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akipata taarifa ya idadi ya wagonjwa waliofanyiwa vipimo 
tangu mashine hiyo ipone kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Mionzi katika 
hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Flora Rwakatare (kulia).
Mkuu wa Idara ya Mionzi katika 
hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Flora Rwakatare akizungumza jambo 
na waandishi wa habari katika chumba cha vipimo vya MRI wakati wa ziara 
ya kushtukiza iliyofanywa na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo 
ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi Kingwangalla, 
Januari 4, 2016.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akiwa ndani ya chumba cha vipimo vya MRI katika hospitali 
ya Taifa ya Muhimbili ya jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya 
kushtukiza, Januari 4, 2016.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akipata maelezo ya mashine mpya ya CT Scan iliyonunuliwa 
hivi karibu na Serikali kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya 
Taifa ya Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru.
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa 
ya Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru (kushoto) akitoa maelezo ya uwezo 
mashine mpya ya CT-Scan iliyonunuliwa na Serikali hivi karibuni ambayo 
hadi kufikia Januari 4, 2016 ikiwa na muda wa siku tatu tangu kuanza 
kutumika hospitalini hapo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo 
ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi Kingwangalla.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akimpongeza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa
 ya Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru baada ya kuona mabadiliko makubwa 
katika hospitali hiyo tangu alipokaimu kiti hicho wakati wa zaiara ya 
kushtukiza katika chumba kilichofungwa mashine mpya ya CT-Scan 
iliyonunuliwa na Serikali hivi karibu na inauwezo mkubwa wa kufanya 
kipimo kwa sekunde 6 na kutoa majibu. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Mionzi 
katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Flora Rwakatare.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi 
Kingwangalla akiwa kwenye dirisha la malipo ya matibabu hospitalini hapo
 wakati wa ziara ya kushtukiza aliyoifanya, Januari 4, 2016.
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na
 Ajali ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya dharura katika 
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Juma Mfinanga akitoa maelezo kwa 
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na 
Watoto, Mhe.  Dk. Hamisi Kingwangalla aliyetembelea kitengo chake, 
Januari 4, 2016. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya 
Taifa ya Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Dk. Hamisi Kingwangalla
 akiendelea kupewa maelezo ya namna wananchi wanavyohudumiwa katika 
kitengo hicho na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali ambaye 
pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya dharura katika Hospitali ya Taifa 
ya Muhimbili, Dkt. Juma Mfinanga.
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na
 Ajali ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya dharura katika 
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Juma Mfinangaakitoa maelezo ya 
ubao maalum unaowaongoza madaktari na wagonjwa wanaohudumiwa katika 
kitengo hicho kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, 
Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Dk. Hamisi Kingwangalla.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Dk. Hamisi Kingwangalla
 akikagua wodi mpya ya wagonjwa mahututi (ICU) ambayo ipo kwenye hatua 
za mwisho kukamilika. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya
 Taifa ya Muhimbili, Prof. Lawrence Mseru  akimtembeza Mh. Naibu Waziri 
kwenye wodi hiyo.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment