Afisa Uendeshaji wa Ofisi za Mpango wa 
Taifa wa Damu Salama zilizopo jijini Dar es Salaam, Bw. Abdu Juma akitoa
 maelezo ya namna wanavyoendesha shughuli zao kwa Naibu Waziri wa Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Hamisi Kingwangalla 
aliyefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi hizo, Januari 4, 2016.
Naibu Waziri wa  Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameagiza 
watanzania wote wasikubali kutozwa rushwa kwa ajili ya damu salama na 
baadala yake kwa mtu atakayefanya hivyo watamchukulia hatua kali.
Kauli hiyo imetolewa mapema Januari 4  
(jana) na Naibu huyo wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, 
Wazee na Watoto, Dkt. Kingwangalla alipofanya ziara katika Ofisi za 
Mpango wa Taifa wa Damu  Salama zilizopo jijini Dares Salaam.
Dk. Kigwangalla amefafanua kuwa, kwa watu
 wote ikiwemo Nesi, Daktari ama mtaalamu wa afya, atakayemtoza mtu damu,
 atachukuliwa hatua kali ikiwemo kufukuzwa kazi.
“Kwa watanzania wote, msikubali kutoa 
rushwa kwa ajili ya damu. Na kama itatokea Nesi ama Daktari ama nani, 
anakuambia ulipie ili upate damu!. Kwa sababu kuna uhaba wa damu kwa 
sasa.. Ripoti kwa Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa ama Daktari Mkuu husika 
ama fika Wizara ya afya moja kwa moja na kuna namba tutaitoa kwa 
watanzania wote  mtupatie ripoti.
Mtu atakayekutoza damu, wewe tuambie, 
huyo tutamfukuza kazi moja kwa moja, hatuwezi kuendekeza watu wa namna 
hii... Serikali inaingia gharama kubwa kukusanya damu kwa watu, Kuna 
watu wanajitolea damu zao bure. Leo wewe nesi ama mganga ukauze damu, 
hilo jambo hatutakubali hata kidogo kwa hiyo natoa rai kwa watanzaia 
hiyo damu ni bure na haiuzwi na usikubali kuuziwa damu hata kidogo.” 
Ameeleza hilo Dk. Kigwangalla.
Awali katika ziara hiyo, Dk. Kigwangalla 
ameipongeza Ofisi ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama  kwa kazi 
wanayofanya na ubunifu waliofikia wa kuhusisha Halmshauri katika 
ukusanyaji wa damu huku wao wakisimamia kudhibiti  viwango vya damu ya 
matumizi kwa watanzania huku akitumia wasaha huo kutoa maelekezo ya 
kuboresha mfumo wa motisha  kwa wanaochangia damu salama ambapo kwa 
wachangiaji damu kuingizwa kwenye mfumo wa kieletroniki wa kuwatambua 
watu wanaochangia damu, kutoa taarifa jinsi damu zao zilivyookoa miasha 
ya wagonjwa na kuwapa motisha ili waweze kuwa wachangiaji endelevu.
“Motisha sio soda na maji kwa 
wanaochangia damu. Motisha ni hata kupewa taarifa kwamba damu yake 
imesaidia kuokoa maisha ya mwanadamu mwenzake aliyekuwa anaumwa ugonjwa 
fulani, hii ni motisha kubwa sana kuliko hata pesa, ama soda ama maji 
yanayotolewa anapochangia damu..
Lakini kama imeshajitokeza mtu kuwa na 
tabia ya kuchangia damu, huyu sio wa kumpoteza, maana yake kuna 
uwezekano mkubwa wa akarudi tena kuchangia damu, mtu huyu ni lazima kuwe
 na mfumo wa kielekrioniki wa komputa wa kumtakia salamu, taarifa na 
anakuwa kwenye database yenu.
 “Mnatakiwa muwe na mfumo wa kumpa 
taarifa pindi damu yake imetumika, ikiwemo kumueleza kuwa damu yako 
imemsaidia Mama mjamzito aliyejifungua na kutokwa damu nyingi, na mtu 
huyo akipata taarifa hiyo ni motisha tosha hivyo ni lazima muwe na huo 
mfumo kutoa motisha zaidi.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla na msafara wake
 wakishuka ngazi kuelekea kukagua idara mbalimbali katika ofisi hizo, 
Januari 4, 2016
Awali akielezwa na Meneja wa kanda ya 
Mashariki katika Ofisi za Mpango wa Taifa wa Damu Salama zilizopo jijini
 Dar es Salaam, Eveline Mgassa kwamba changamoto zilizopo katika 
upatikanaji wa damu nchini ni halimshauri kutenga bajeti za kutosha kwa 
ajili ya huduma hiyo, Kwa hatua hiyo, Dk. Kigwangalla ameziagiza 
Halmshauri zote nchini kuhakikisha zinatenga bajeti za kutosha 
ilikusapoti mpango wa damu salama.
Katika hilo  Dk. Kigwangalla ameapa 
kuwashughulikia wale wote  watakaozembea na kuwachukulia hatua kali Ma 
DMO, Wakurugenzi na kushtakiwa kwa mamlaka zilizopo na kufukuzwa kazi.
“Naziagiza Halmashauri zote kuhakikisha 
zinatenga bajeti za kusapoti mpango wa ukusanyaji damu salama. Na 
Halmashauri zitakazoshindwa, DMO na Mkurugenzi wake tutahakikisha 
tunawashtaki kwa mamlaka zilizowateua ili uteuzi wao ukome mara moja. 
Maana hatuwezi kuacha akinamama wajawazito wapoteze damu wakati wa 
kujifungua, watu wanaopata ajali wapoteze maisha kwa sababu ya watu 
hawataki kutimiza wajibu wao.
Hilo haliwezi kukubalika, Mfumo wa hali 
ya damu kwa Tanzania kwa sasa unatisha. Kwa sasa nchi inakiwango cha 
chini mno, tokea wafadhili wajiondoe katika hili. Ni lazima tuwe makini 
sana maana leo mzima kesho umepata ajali, umepasuka mfupa wa kwenye paja
 damu nyingi zimemwagika unahitaji damu!!
Kwa upande wa watu wote wanaopata damu 
salama nchini,  huduma hiyo wanazipata bure kwani damu hizo ni za 
Serikali, Hata hivyo mifuko na vitu vinavyotumika kuhifadhia damu hiyo 
vina gharama kubwa.
“Damu inatolewa bure na serikali. Mtambue
 kuwa, vifaa vya kutunzia damu hii ni gharama kubwa. Hivyo mifuko 
mashirika ya Bima, na mashirika mengine kuanzia leo kutazama namna ya 
kulipa gharama za vifaa vya utunziaji damu hizo. Damu ni bure, lakini 
mfuko ule wa kutunzia ile damu ni gharama kubwa sana na hata vifaa vya 
kupimia damu ile nayo ni gharama kubwa hivyo walipie kwa kila damu 
watakayochukua.” Alieleza Dk. Kigwangalla.
Meneja wa kanda ya Mashariki Ofisi za 
Mpango wa Taifa wa Damu Salama zilizopo jijini Dar es Salaam, Eveline 
Mgassa (mwenye miwani) akielezea utaratibu wa ukusanyaji wa damu 
unavyofanyika kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, 
Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla aliyefanya ziara ya kushtukiza
 katika ofisi hizo, Januari 4, 2016 jijini Dar.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla (aliyeipa 
mgongo kamera) akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Uendeshaji wa Ofisi 
za Mpango wa Taifa wa Damu Salama zilizopo jijini Dar es Salaam, Bw. 
Abdu Juma ya namna wanavyopokea watu wanaofikia kuchangia damu kwa hiari
 na kuhifadhiwa kwenye benki hiyo yaTaifa ya Damu Salama, alipofanya 
ziara ya kushtukiza, Januari 4, 2016 katika ofisi hizo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Hamisi Kingwangalla akitoa mkono wa 
pongezi kwa wananchi walioonyesha uzalendo kwa kufika katika ofisi za 
Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Januari 4, 2016 na kuchangia damu kwa 
hiari yao ambapo mmoja kati yao alisema hii ni mara yake ya nne na ni 
utararibu aliojiwekea.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Hamisi Kingwangalla akisalimiana na 
kumpongeza mmoja wa wananchi (jina lake halikuweza kupatikana) aliyefika
 kuchangia damu kwa hiari, Januari 4, 2016 katika makao makuu ya ofisi 
za Mpango wa Taifa wa Damu Salama.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Hamisi Kingwangalla akiwa ndani ya 
maabara ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama alipofanya ziara ya kushtukiza
 kwenye ofisi hizo, Januari 4, 2015  jijini Dar es Salaam.
Afisa Uendeshaji wa Ofisi za Mpango wa 
Taifa wa Damu Salama zilizopo jijini Dar es Salaam, Bw. Abdu Juma 
akimwonyesha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na 
Watoto, Dkt.Hamisi Kingwangalla moja ya damu ambayo ni maalum kwa wamama
 wajawazito wakati wa kujifungua zilizohifadhiwa kwenye jokofu katika 
mabara hiyo.
Mmoja wa watumishi katika maabara ya 
ofisi za Mpango wa Taifa wa Damu Salama (ambaye jina lake halipatikana) 
akiendelea kutekeleza majukumu yake kama alivyokutwa na mpiga picha 
wetu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Hamisi Kingwangalla akisaini vitabu 
vya wageni nje ya ofisi za Mpango wa Taifa wa Damu Salama zilizopo 
jijini Dar es Salaam, Januari 4, 2016 wakati alipofanya ziara ya 
kushtukiza katika ofisi hizo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Hamisi Kingwangalla akizungumza na 
waandishi wa habari baada ya kufanya ziara ya kushtukiza na kuzungikia 
vitengo mbalimbali katika ofisi za Mpango wa Taifa wa Damu Salama jijini
 Dar es Salaam.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment