WAZIRI wa 
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Mkurugenzi 
Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro
 na kuzungumzia fursa mbalimbali za uwekezaji nchini hususan katika 
sekta ya Nishati.
Muro alimtembelea Waziri Muhongo na kueleza nia ya Kampuni yake 
kuwekeza kwenye mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirishia mafuta kutoka 
Dar es Salaam hadi Mwanza na vilevile uwekezaji kwenye mradi wa ujenzi 
wa nguzo za umeme za zege. 
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akimsikiliza
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, 
Elisante Muro wakati wa kikao cha kujadili fursa za uwekezaji.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) 
akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mtendaji wa 
Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro (hayupo 
pichani) ambaye alimtembelea Waziri huyo kuzungumzia fursa za uwekezaji 
kwenye sekta ya nishati nchini. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu- 
Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo akifuatiwa na Naibu Katibu 
Mkuu- Madini, Profesa James Mdoe.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) 
akizungumza jambo wakati wa kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya 
Africommerce International Limited, Elisante Muro (hayupo pichani) 
wakati wa kikao cha kujadili fursa za uwekezaji. Katikati ni Naibu 
Katibu Mkuu- Madini, Profesa James Mdoe na wa kwanza kulia ni Naibu 
Katibu Mkuu- Nishati, Dkt. Mhandisi, Juliana Pallangyo
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment