Mjasiliamali
 wa mjini Bukoba Adamu Hemed akipokea cheti kutoka kwa meneja biashara 
wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Mohamedi kabeke baada ya 
kuhudhuria mafunzo ya ujasiliamali yaliyoendeshwa na mradi wa Airtel 
FURSA kwa Zaidi ya vijana 200. kati ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini 
bukoba Bw, Frabius Ngemela na Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando 
mwishoni mwa wiki hii mkoani Kagera.
 .Mkulima
 wa mboga mboga kutoka Bukoba mjini Agnetha Frenk akipokea cheti toka 
kwa meneja wa biashara Airtel BUkoba Mohamed kabeke baada ya kuhudhuria 
mafunzo ya ujasiliamali yaliyoendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya 
Airtel mjini Bukoba kati ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini bukoba Bw, 
Frabius Ngemela na anaefuata ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson 
Mmbando. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na 
kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 mkoani Kagera.
Mkazi
 wa mtaa wa Nshambya mjini Bukoba Janath Shafi anayejishughulisha na 
biashara ya ufugaji wa mbuzi akipokea cheti toka kwa meneja wa biashara 
Airtel BUkoba Mohamed kabeke baada ya kuhudhuria mafunzo ya ujasiliamali
 kwa vijana yaliyandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi 
ya Airtel mkoani Kagera. Cheti baada ya kuhudhuria mafunzo ya 
ujasiliamali yaliyoendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, 
Katikati ni mwalimu wa mambo ya ujasiliamali ambae pia ni Afisa 
ujasilimali wa VETA mjini bukoba Bw, Frabius Ngemela na anaefuata ni 
Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando. Semina hiyo ilifanyika 
mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 
mkoani Kagera.
 Kijana
 anayejishughulisha na ufugaji wa kuku kutoka Kijiji cha Katoka Wilaya 
ya Bukoba Vijijini Lucas Joseph akipokea cheti toka kwa meneja wa 
biashara Airtel BUkoba Mohamed kabeke baada ya kuhudhuria mafunzo ya 
ujasiliamali kwa vijana yaliyandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu 
za mkononi ya Airtel mkoani Kagera. Katikati ni mwalimu wa mambo ya 
ujasiliamali ambae pia ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini bukoba Bw, 
Frabius Ngemela na anaefuata ni meneja uhusiano wa Airtel Jackson 
Mmbando. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na 
kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 mkoani kagera.
Baadhi
 ya washiriki wa mafunzo ya ujasiliamali yaliyofanyika mjini Bukoba 
yaliondaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Airtel 
kupitia mpango wake wa fursa tunakuwezesha. Semina hiyo ilifanyika 
mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 
mkoani kagera
· Bukoba zaidi ya wajasiliamali vijana 200 wanolewa na Airtel Fursa
KAMPUNI
 ya mawasiliano ya simu za mkononi airtel imewataka watanzania 
kuchangamkia fursa zilizopo kwa kufanya ujasiriamali kwa mtazamo mpana 
kwa lengo la kuondokana na umasikini au maisha duni yasiyo na kipato 
maalum.
Hayo 
yamesemwa na mwalimu wa mambo ya ujasiliamali ambae pia ni Afisa 
ujasilimali wa VETA mjini Bukoba Bw, Frabius Ngemela kwa zaidi ya 
wajasiliamali 200 waliohuduria semina ya ujasiliamali ya Airtel Fursa 
BUKOBA akiwataka vijana wajasiliamali kutumia ujuzi na maarifa katika 
kuboresha miradi yao kama njia mojawapo ya kukabiliana na suala la 
umasikini na kuwataka wajasiliamali hao kutokata tamaa ya maisha badala 
yake waongeze juhudi katika uzalishaji mali bila kuogopa vikwazo ili 
kujikomboa.
Airtel
 Fursa imekuja Bukoba leo kuwaambia msikate tamaa, nawafundisha leo 
kuvitambua vikwazo na msiviogope katika shughuli zenu, mkashirikiane na 
mradi wa Airtel Fursa ili kujikwamua.
Kwa 
upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alieleza “Airtel 
Fursa sio tu tunawasaidia vijana kuzitambua fursa pia tunawapatia mitaji
 na vitendea kazi muhimu ambavyo vimekua ni vikwazo vya kutimiza malengo
 yako ili uweze kuzalisha zaidi na kusaidia jamii zao.
“Hadi 
sasa tumeshazunguka mikoa zaidi ya 12 ndani ya miezi hii minne 
tukiwaeleza vijana jinsi wanavyoweza kukamata FURSA na kuwasaidia 
kupitia warsha kama hizi pia kuwapatia vitendeakuzalis kazi na vifaa 
mbalimbali waweze kuzalisha zaidi” alisema Mmbando.
wakiongea
 mara baada ya kupatiwa elimu ya ujasilimali baadhi ya wajasiliamali 
wadogo Peace Ruben MJASIRIAMALI, alisema licha ya kupatiwa elimu hiyo 
bado wanakabilina na changamoto mbalimbali ikiwemo mitaji ya kuendeshea 
biashara zao ambapo pia wametumia nafasi hiyo kuiomba kampuni ya airtel 
kwa kutumia mradio wao wa Airtel fursa kuwapatia mitaji itakayo wasaidia
 kuendesha biashara zao.
“Mi 
kazi yangu ni kufuma vitambaa na nguo za kuzuia baridi kwa watoto , 
wateja wangu wanapatikana kwa urahisi hapa bukoba na nje ya bukoba yaani
 hapo mpakani mwa Tanzania na Uganda lakini tatizo ni vitendea kazi vya 
kutosha ili kuongeza uzalishaji, ikiwa Airtel Fursa itanitoa nitafurahi 
sana” alieza Peace Ruben
 
 
 
 
 
 





 
 
0 comments:
Post a Comment