Mmoja
 wa wateja wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Kakili Juma (wa pili kushoto) 
akiokota karatasi yenye jina la mshindi wa droo ya mwisho na kubwa ya 
kampeni ya akaunti ya malengo ya Benki ya Exim Tanzania iliyofanyika 
makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni kwa 
wiki.Wanaoshuhudia kushoto ni pamoja na Meneja Bidhaa ya benki hiyo, Bw 
Aloyse Maro, Mwakilishi kutoka Bodi ya Taifa michezo ya kubahatisha 
nchini (GBT), Bw Bakari Maggid, Meneja Masoko wa benki hiyo Bw. 
Abdulrahman Nkondo pamoja na Ofisa wa benki hiyo Bw. George Musetti.
BENKI
 ya Exim Tanzania imeendesha droo yake ya mwisho na kubwa ya kampeni ya 
akaunti ya malengo huku mteja wa benki hiyo Bw.Dileshkumar Solanki mkazi
 wa wa jijini Dar es Salaam akiibuka mshindi na hivyo kujishindia gari 
ndogo aina ya Toyota IST. 
Kampeni
 hiyo ilizinduliwa mwezi Mei mwaka huu ambapo kupitia kampeni hiyo benki
 hiyo imekua ikitoa zawadi mbalimbali za kila mwezi zikiwemo simu aina 
ya iPhone 6 kwa wateja waliobahatika kuibuka washindi kutoka maeneo 
mbalimbali hapa nchini. 
Akizungumza
 kwenye hafla fupi ya uendeshaji wa droo hiyo iliyofanyika mwishoni mwa 
wiki kwenye makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam, Meneja 
Bidhaa wa benki hiyo Bw Aloyse Maro alisema benki hiyo imeridhishwa na 
mwitikio mkubwa kutoka kwa wateja wake wakati wote wa kampeni hiyo 
inayolenga kuhamasisha utamaduni wa kuweka akiba miongoni mwa 
watanzania. 
“Kampeni
 hii imekuwa ni yenye mafanikio. Imepokelewa kwa mwamko mkubwa kutoka 
kwa wateja wetu hatua ambayo tumeitafsiri kwamba ni wazi wateja wetu 
wananufaika na wanafurahia huduma zetu,’’ alisema Bw Maro muda mfupi 
baada ya kufanyika kwa droo hiyo iliyosimamiwa na Bodi ya taifa michezo 
ya kubahatisha nchini (GBT) 
Bw.
 Maro aliongeza kuwa sambamba na zawadi hizo kampeni hiyo inaambatana na
 utoaji wa riba nzuri zaidi kwa wateja wanaofungua akaunti hiyo ya 
malengo. 
“Hatujaishia
 tu kwenye kutoa zawadi hizi kwenye kampeni hii bali tulihusisha pia 
utoaji wa riba nzuri zaidi kwa wateja wanaofungua akaunti yetu ya 
malengo,’’ alibainisha. 
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment