Meneja
 Mawasiliano na Mahusiano wa Efm Radio, Denis Ssebo akizungumza na 
wandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya wasanii zaidi ya 50 wa Bongo 
Movie akiwamo Steve Nyerere, Wema Sepetu na Vicent Kigosi (Rey) 
wataungana na kituo cha redio cha EFM na Benki ya DTB kufanya usafi 
Desema 9 mwaka huu. Usafi huo utaanzia katika barabara ya Morocco hadi 
Magomeni, mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni 
Mkuu wa Bidhaa na Masoko wa benki ya Diamond Trust Bank (DTB), Sylvester
 Bahati.
 Mkuu 
wa Bidhaa na Masoko wa benki ya Diamond Trust Bank (DTB), Sylvester 
Bahati akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya usafi 
ni nguzo moja wapo katika benki hiyo na si kwa ajili ya agizo la Rais 
John magufuli bali ni zoezi endelevu, kulia ni Meneja Mawasiliano na 
Mahusiano wa Efm Radio, Denis Ssebo.
Wandishi
 wa habari wakimsikiliza Meneja Mawasiliano na Mahusiano wa Efm Radio, 
Denis Ssebo, mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam
Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii.
 WASANII  wa 
Bongo Movie zaidi
 ya 50 akiwamo Steve Nyerere, Wema Sepetu na Vicent Kigosi (Rey) 
wataungana na kituo cha redio cha EFM na Benki ya DTB kufanya usafi 
Disemba 9 mwaka huu.
Akizungumza
 leo jijini Dar es Salaam Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EFM, 
Denis Ssebo, amesema usafi huo utaanzia katika barabara ya Morocco hadi 
Magomeni.
Ssebo 
amesema katika usafi huo EFM, DTB pamoja na wasanii hao watashirikiana 
na viongozi mbalimbali walioko madarakani pamoja na wakazi wa Kinondoni 
chini ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda.
Kauli 
mbiu ya siku hoyo isemayo ‘Naona aibu kuishi na uchafu’ huku tukiunga 
kauli mbiu ya kinondoni ‘Usafi uanze na mimi’ endapo kila mmoja 
atatambua umuhimu wa usafi wake, mazingira yake tutaweza kwa pamoja 
kulimaliza tatizo la uchafu nchini,”amesema Ssebo. 
Kwa 
upande wake mwakilishi wa DTB Silvesta Bahati alisema usafi ni nguzo 
moja wapo katika benki hiyo na si kwa ajili ya agizo la Rais John 
magufuli bali ni zoezi endelevu.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment