Afisa
 Uhusiano wa Airtel, Dangio Kaniki (kushoto) na Meneja uhusiano wa 
Airtel, Jackson Mmbando (katikati) wakipima uzito wa kuku wa kienyeji 
wanaofugwa kisasa na kijana Mohamed Kigumi (kulia), anayeishi Kiluvyia 
jijini Dar Es Salaam baada baada ya kutembelewa nyumbani kwao na kuona 
maendeleo aliyoyapata baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia mpango wa 
Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ miezi sita iliyopita.
Afisa
 Uhusiano wa Airtel, Dangio Kaniki (kulia) na Meneja uhusiano wa Airtel,
 Jackson Mmbando (katikati) wakitazama maandalizi ya utunzaji wa kuku wa
 kienyeji wanaofugwa kisasa na kijana Mohamed Kigumi (kulia), anayeishi 
Kiluvyia jijini Dar Es Salaam baada baada ya kutembelewa nyumbani kwao 
na kuona maendeleo aliyoyapata baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia 
mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ miezi sita iliyopita.
Kijana
 Mohamed Kigumi anayeishi Kiluvyia jijini Dar Es Salaam akiwaelekeza 
meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando (katikati) na afisa Uhusiano 
wa Airtel, jinsi anavyoendesha ufugaji wake wa kuku baada ya kumtembelea
 nyumbani kwao na kuona maendeleo aliyoyapata baada ya kuwezeshwa na 
Airtel kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ miezi sita 
iliyopita.
VIJANA
 wengi wana ndoto za kujiletea maendeleo lakini wanashindwa kutimiza 
ndoto zao kutokana na kukosa elimu sahihi na kutokuwa na mitaji ambayo 
ingewawezesha kujiunga kwenye miradi ya ujasiriamali.
Kampuni
 ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mradi wake wa Airtel FURSA imeiona
 changamoto hiyo na kuamua kuwafikia vijana mbali mbali hapa nchini 
akiwemo kijana Mohamed Kigumi ambaye mpaka sasa ameonesha jitihada za 
kujikwamua na umaskini kwa kuwawezesha kupata mitaji ama vifaa 
vitakavyotimiza ndoto zao.
Akiongea
 katika kijiji cha kiluvya, Muhamed Kigumi ambaye anajishuhulisha na 
ufugaji wa kuku wa kienyeji, amesema licha ya kuanza kazi hiyo kwa muda 
mrefu lakini sasa ameanza kuona mafanikio makubwa katika kazi yake 
kutokana na kujengewa mabanda ya kisasa ya kufugia kuku wake na mfuko wa
 Airtel FURSA tofauti na hapo awali ambapo alikuwa akifugia kukuwake 
kwenye mazingira magumu.
Amesema
 mabanda ya kisasa aliyojengewa na mfuko wa Airtel FURSA pamoja na 
kupatiwa msaada wa kuku, maisha yake yamebadilika kwani sasa ameamua 
kujiajiri katika kazi hiyo na kumuwezesha kusaidia familia na kuuomba 
mfuko huo kendelea kuwasaidia vijana wengine hapa nchini.
Akiongea
 katika mabanda ya kuku ya kijana huyo alipomtembelea hapo jana, meneja 
uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando amesema kuwa mpango wao wa Airtel 
FURSA umefurahishwa na jitihada za kijana huyo ambapo wamemtembelea bila
 kumpa taarifa lakini wamebaini kuwa msaada waliompatia kijana Mohamed 
umeweza kuyabadilisha maisha yake kutokana na kuwa makini na kazi yake.
Mmbando
 aliongeza kwa kusema, mpango wa kuwasaidia vijana wenye umri kati ya 
miaka 18-24 uitwao Airtel FURSA umeanzishwa na mtandao wa simu za 
mikononi wa Airtel ili kuwasaidia vijana wa Tanzania wenye ndoto zao ili
 kuweza kuzitimiza ndoto zao kwa kuwawezesha kwa kuwapatia elimu ya 
biashara na nyenzo za kufanyia kazi.
 
 
 
 
 
 



 
 
0 comments:
Post a Comment