Kaimu
 Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Philip Mpango 
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano na 
Kaimu
 Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Philip          
                                     Mpango jijini Dar es Salam leo.
Na ChalilaKibuda,Globu ya Jamii
BAADA
 ya Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa kufanya ziara ya kushitukiza katika 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kubaini upotevu wa Makontena 329, 
mapya yaibuka kwa Makampuni 43 kuhusika kukwepa kodi ya Sh.Bilioni 12.6 
katika Bandari Kavu inayomilikiwa na Said Salim Bakh ressa.
Akizungumza
 na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kaimu Kamishna Mkuu wa
 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Philip Mpango amesema kuwa 
kampuni hizo 43 zilipitishiwa Kontena katika Bandari Kavu ya Said Salim 
Bakhressa na kutaka ndani ya siku sita kuanzia leo kampuni zote ziwe 
zimeshalipia kodi kutokana na idadi ya kontena.
Dk.
 Mpango amesema katika kampuni ambazo zilizokwepa kodi ambazo 
zilipitisha Kontena 329 wameshalipa zaidi ya Sh. Bilioni Tano(5) ambapo 
wanatakiwa kulipa kodi iliyobaki kuweza kumaliza kodi ya Sh.Bilioni 12.6
 kwa kipindi alichoweka Rais Dk .John Pombe Magufuli. 
Amesema
 kuwa hatilafu za kupotea kwa makontena hayo, kazi hiyo walishakuwa 
wameanza kwa bahati mbaya Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa Majaliwa 
aliwawahi wakati alipofanya ziara katika mamlaka hiyo.
Kampuni
 zilizokwepa Kodi ya mapato kwa makontena 329 ni Lotai Steel Tanzania 
LTD yenye makontena 100,Tuff Tyres Centre Company kontena 58 Binslum 
Tyres Company LTD, Kontena 33, Tifo Global Mart (Tanzania) Company 
Limited Kontena 30,IPS Roofing Campany Ltd Kontena 20,Rashywheel Tyre 
Center Com.Ltd Kontena 12, Kiungani Trading Company Ltd 10 Homing 
International Limited Kontena 9, Red East Building Kontena Saba,Tybat 
Trading Co Ltd, Kontena Tano,Zing Ent Ltd,Kotena Nne,Juma Kassem Abdul, 
Kontena Tatu, Salum Continental Co.Kontena Mbili, Zuleha Abbas Ali 
Kotena Mbili na Snow Leopard Building Kontena mbili na waliobaki 
walikuwa na kontena moja moja.
Hata
 hivyo TRA imewasimamisha kazi watu 35 wakiwemo 27 waliokamatwa katika 
geti namba tano ambao hadi sasa wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano na
 uchunguzi .
Aidha amewataka wafanyakazi kuwasilisha mali zao ili kuweza kuangalia uwezo wake katika utumishi kama zinaendana na umiliki huo.
 
 
 
 
 
 


 
 
0 comments:
Post a Comment